Pages

Friday, February 8, 2013

vijana wahitimu mafunzo ya awali ya kijeshi jkt kanembwa wilayani kibondo mkoani kigoma


Vijana 571 operation sensa 2012  wa kikosi cha jeshi namba  824 wamemaliza mafunzo ya awali ya kijeshi katika kambi ya jkt Kanembwa wilayani kibondo mkoani kigoma  wakiwa wamepata mafunzo mbali mbali ya kijeshi , uzalishaji , ufundi stadi , ujasiliamali pamoja na  kutoa msaada wa shughuli mbali mbali za kijamii
 Mgeni lasmi katika sherehe hizo za kumaliza mafunzo ya awali kikosi 824 jkt kanembwa alikuwa mkuu wa mkoa wa kigoma kanali mstaafu sahehe isa machibiya na alianza kwa ukaguzi wa gwaride lililoandaliwa na vijana hao
 Baada ya ukaguzi huo vijana hao walikula kiapo mbele ya mgeni lasimi na wageni mbali mbali walioambatana nae wakiwemo wakuu wa wilaya za mkoa wa kigoma pamoja na viongozi wa kisiasa wageni waalikwa  na viongozi wa kidini
 Baada ya zoezi hilo mkuu wa kikosi 824meja elasmos Bwegoge akitoa hotuba kwa mgeni lasimi amesema kuwa jeshi la kujenga taifa linayo dira na dhima katika kuwapokea na kuwafunza vijana kutoka sehemu mbali mbali bila kujali kabila
 Mjumbe wa baraza la ngumi za lidhaa nchini BFT na mwakilishi wa wananwake maendeleo ya vijana na ajila kwa wachezaji bi Zuena idd omary kipingu amewataka vijana hao kuendeleza hishima na nidhamu waliyoipata katika mafunzo yao
 Nae mkuu wa mkoa wa kigoma kanali mstaafu salehe issa machibiya ambaye alikuwa mgeni lasmi katika sherehe hizo akitoa hotuba yake kwa wageni waalikwa na vijana wanaomaliza mafunzo  amewataka vijana kuwa na moyo wa kujituma na kujitolea ili waweze kulitumika taifa kwa moyo wote
 Vijana 571 operation sensa 2012 wamemaliza mafunzo ya awaliya kijeshi katika kambi ya jkt kanembwa ambapo wasichana walikuwa 105 na wavulana 466 na vijana 9 wakishindwa kumaliza mafunzo hayo kutokana na sababu mbali mbali

vijana walipata nafasi ya kupiga picha na mgeni lasmi mkuu wa mkoa wa kigoma salehe issa machibiya

Mjumbe wa baraza la ngumi za lidhaa nchini BFT na mwakilishi wa wananwake maendeleo ya vijana na ajila kwa wachezaji bi Zuena idd omary kipingu alikuwepo kutoa sapoti yake


mgeni lasmi ruten kanali Salehe Issa Machibiya akikagua gwaride
maandamano haramu
mkuu wa mkoa wa kigoma kanali mstaafu Salehe Issa machibya



namna ya kuvuka mto uliovunjwa daraja
vikwazo


kwa pamoja tulijenge taifa letu

No comments:

Post a Comment