Pages

Friday, November 15, 2013

Baraza la madiwani wilayani kibondo mkoani kigoma limeketi ikiwa ni kikao cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2013/ 2014








Halmashauri ya wilaya ya kibondo mkoani kigoma imeidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 3 na milioni 347 katika mwaka wa fedha 2013/ 2014 kutoka serikali kuu na wahisani mbali mbali wa maendeleo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoko chini ya kamati ya elimu afya na maji

Mwenyekiti wa kamati ya elimu afya na maji bw Ali Amini Gwanko Mpondamali ameyasema hayo wakati akisoma taarifa ya kamati hiyo katika baraza la madiwani lililoketi leo katika ukumbi wa vijana na kuongeza kuwa fedha hizo ni sawa na asilimia 57.5 ya bajeti yote iliyoidhinishwa

Aidha bw Gwanko amesema kuwa halmashauri ilikuwa imebaki na salio ishia kwa mwaka wa fedha 2012/2013 kiasi cha shilingi bilioni 3 na milioni 525 hivyo pesa itakayotekeleza miradi mbali mbali katika kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2013/2014 itakuwa zaidi ya shilingi bilioni 6

Amesema kuwa katika utekelezajaji wa miradi mbali mbali kamati ya elimu, afya na maji kwa mwaka wa fedha uliopita ilikabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo kuchelewa kuanza kwa mfumo wa EPICA na hivyo kushindwa kufanya malipo kwa wakandarasi wenye mitaji midogo hivyo kukwamisha kazi

No comments:

Post a Comment