Pages

Saturday, March 15, 2014

mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya kati yateketeza bidhaa feki kibondo



Mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya kati imeteketeza tani moja na nusu ya  bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu bidhaa ambazo zimekusanywa kutoka maduka mbali mbali yaliyoko katika wilaya za kakonko na kibondo

Mkaguzi wa chakula kutoka mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya kati bw Abel Dauda  amesema kuwa ofisi ya mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya kati katika kutekeleza mpango kazi wake kwa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2013/14 imefanya ukaguzi katika halmashauri za wilaya ya kibondo na kakonko kwa kushirikiana na ofisi za waganga wakuu wa halmashauri husika

Kwa upande wake afisa afya mazingira wilayani kibondo bw joseph kalobagwa amesema kuwa elimu huotolewa kila wanapotembelea maduka mbali mbali ili kuhimiza kuacha tabia ya kuagiza bidhaa zisizo faa kwa matumizi ya binadamu

Mmoja wa wafanyabiashara wilayani kibondo bw musa hamisi ameitaka mamlaka ya chakula na dawa kudhibiti wafanyabiashara wakubwa kwa kuwa wao ndio husambaza bidhaa zisizo na ubora kwa wafanya biashara wadogo

Ukaguzi huo uliofanywa na TFDA kanda ya kati ulilenga kuangalia utekelezaji wa sheria ya chakula dawa na vipodozi namba moja ya mwaka 2003 katika udhibiti wa ubora usalama na ufanisi wa bidhaa za chakula dawa  vipodozi na vifaa tiba 

No comments:

Post a Comment