Pages

Thursday, November 21, 2013

mme aua mke mtoto akaa na maiti yaya mama yake kwa siku tatu



 
mkuu wa jeshi la polisi wilayani kibondo bw Marko Joshua akifungua mlango katika nyumba aliyokutwa marehemu
 
mwili wa marehemu kama ulivyokutwa chumbani
mtoto aliyeishi ndani na maiti ya mama yake kwa muda wa siku tatu akiwa amebebwa na babi yake

 
pamoja na kukutwa akiwa hai pembeni ya marehem mama yake lakini inaonekana nae alipata suruba kiasi fulani

 
baba mzazi wa kijana aliyetekeleza mauaji

Mwanamke Mmoja Mkazi wa Kijiji cha Mpevyi Kata  ya Busagara Wilayani Kibondo ameuawa kikatili kwa kunyongwa  shingo hadi kufa na  mumewake na mwili wake kukutwa umeharibika vibaya baada ya kuterekezwa kwa kufugiwa ndani kwa siku 3, na mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 5.

Taarifa za awali kutoka kamati ya Ulinzi na usalama ya Kijiji hicho imemtaja aliyeuawa kuwa ni Bi.Anerth Shabani mwenye umri wa miaka 22, akiwa na mtoto wake Lahabu Bugaru mwenye umri wa miaka 5 ambaye amekutwa akiwa hai huku akiwa  amejeruhiwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu za usoni na mapajani.


Akizungumza na kibondo moto Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bw.  Felix Kabuti amesema tukio hilo limetukia usiku wa November 16 mwaka huu, Nyumbani kwake ambapo imeelezwa kuwa marehemu Anerth shabani ameuawa na mumewake shedrak yoram Chales kwa kumunyongwa kisha kuulaza mwili wake kitandani na yeye kutokomea kusikojulikana baada ya kutekeleza unyama huo

.
Naye diwani wa kata ya Busagara Bw. Godwin Sibanilo amesema awali alipata taarifa kutoka kwa wananchi iliyoashilia kuwepo kwa harufu kali kutoka katika nyumba hiyo ambapo kwa kushirikiana na viongozi walifanikiwa kubomoa mlango na kuingia ndani ambapo walikuta mwili wa mwananke huyo na mtoto Lahabu bugaru aliyekuwa ameulalia mwili wa mama yake.


Ndugu wa mwanamke huyo aliyenyongwa waliruhusu daktari kufanya uchunguzi wa kifo hicho kimesababishwa na nini ambapo pia waliruhusu askari kufanya uchunguzi wao lakini wamegomea mwili huo kuzikwa kwa madai kuwa mwanaume huyo hakuwa ametoa mahali wakati alipomuoa binti yao

No comments:

Post a Comment