Pages

Monday, February 25, 2013

mahafari ya tisa shule ya sekondari ya wasichana Bon Konsil Mabamba Kibondo

Walimu wametakiwa kuiona kazi ya ualimu  kuwa ni wito  ili kufanya kazi hiyo  kwa bidii  na moyo wa kujituma pamoja na nia ya kuwasaidia wanafunzi hali itakayosaidia kuinua kiwango cha elimu na ufauru mzuri

Ameyasema hayo mgeni lasmi  padre Christopher Ndizeye paroko wa parokia ya Kibondo katika mahafari ya 9 ya kidato cha sita shule ya sekondari ya wasichana  Bon Konsili  yaliyofanyika katika ukumbi wa shule hiyo iliyoko kata ya mabamba wilayani Kibondo

Aidha padre Ndizeye amesema kuwa mwalimu anapaswa kujitoa kwa ajili ya shule na wale anaowafundisha hali itakayosaidia wanafunzi kupenda masomo yao na hatimae kuinua kiwango cha taaruma


Mkuu wa shule hiyo ya wasichana bon konsil sisita Generoza Mpilirwe amewataka Wazazi na walezi  kuacha tabia ya kuwalaumu walimu pale watoto wao wanapokuwa wamefeli mtihani  bali wajenge tabia ya kuwafunza nidhamu kwa kuwa nidhamu ndio msingi wa maendeleo mazuri  ya mwanafunzi

Katika risala iliyoandaliwa na wahitimu na kusomwa na Tekla mchunguzi kwa kiingereza  kisha ikasomwa na Juliana Bagamba  kwa Kiswahili wamesema kuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi zinazopelekea kushindwa kujisomea kwa wakati likiwemo suala zima la ukosefu wa nishati ya umeme
 
Mkuu wa wilaya ya Kibondo ambaye alikuwa mgeni mwalikwa katika mahafari hiyo ya kidato cha sita ameahidi kutatua tatizo la umeme ambapo baada ya kukamilika katika mji wa kibondo hatua itakayofuata ni kupeleka nishati hiyo katika kata ya Mabamba na Busunzu

Mzee faransisi mkosamali yeye aliwakilisha wazazi katika sherehe hizo za kuwaaga wahitimu wa kidato cha sita bon konsil


Wanafunzi 37 kati ya 41 walioanza kidato cha tano  wamehitimu elimu ya kidato cha sita katika shule ya wasichana Bon Konsil wakiwa wamefanikiwa kufanya vizuri katika mitihani yao ya moko wakshika nafasi ya pili kimkoa MWISHO

















No comments:

Post a Comment