Pages

Sunday, September 15, 2013

serikali ya kijiji kibondo mjini imepania kujiuzuru uongozi ifikapo september 28 kufuatia kutoelewana na uongoz wa halmashauri ya wilaya hiyo



Viongozi na wajumbe wa Halmashauri ya kijiji cha kibondo mjini wametoa taarifa ya kujiuzuru nafasi yao kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya kibondo ifikapo septemba 28 mwaka huu  ikiwa halmashauri hiyo  haitatafuta  ufumbuzi wa migogoro iliyopo kati ya kijiji hicho na halmashauri

Mwenyekiti wa kijiji cha kibondo mjini bw Robert Ntendeli ameiambia KIBONDO MOTO kuwa uamuzi huo ulitolewa na wajumbe wa  kikao kilichoketi agost 30 , 2013 na kuthibitishwa na wajumbe 19 septemba 2 mwaka huu huku wajumbe watano wakiwa ndio pekee hawakusaini barua hiyo

Bw Ntendeli amesema kuwa wajumbe wa halmashauri ya kijiji cha kibondo mjini wamefikia hatua ya kutaka kujiuzuru kwa sababu zipatazo sita ambapo sababu hizo ni pamoja na juhudi za halmashauri ya kijiji kupendekeza na kufuatilia utayari wa mamlaka ya mkurugenzi kufanya marekebisho stahiki ili kuwezesha halmashauri ya kijiji kutimiza wajibu wake wa kuchochea maendeleo ya kijiji hazikupewa umuhimu stahiki na hivyo kuikatisha tamaa

Usajili wa kijiji cha kibondo mjini haukuzingatia matakwa muhimu ya kisheria katika fungu la 22 la sheria namba 7 ya mwaka 1982 la uwepo wa ardhi yenye mipaka inayojulikana na jitihada za kuanzisha mamlaka ya mji mdogo kwa misingi ya mafungu ya 27 na 28 ya sheria ambalo ndilo lilikuwa suruhisho

Sababu nyingine ni mji wa kibondo haukustahili kuwa na halmashauri ya kijiji kinyume na sheria baada ya kutokuwa na ardhi yake na kulazimika kutawaliwa kwa sheria za ardhi mbili tofauti namba 4 na 5 za mwaka 1999 hali ambayo kiutendaji inatatanisha

Bw ntendeli amesema kuwa sababu nyingine ya kutaka kujiuzuru ni kuwa halmashauri ya kijiji imeshindwa kuendelea na utendaji wa kuingiliana na ofisi ya mkurugenzi ikiwa ni pamoja na ugawaji wa ardhi , uuzwaji wa majengo na utekelezaji hafifu wa miradi inayofanywa kwa masirahi binafsi katika eneo la mji bila kushirikishwa

Halmashauri ya kijiji pia inahofia kuwajibishwa na mkutano mkuu wa kijiji kwa misingi ya sheria katika vifungu vya 142 na 143 vya sheria kwa kutotimiza wajibu wao huku wakizuwiya uwezekano wa kuendelea kwa kijiji kwa kuhofia kuwaudhi viongozi wanaokinzana nao

Sababu ya mwisho ni kwamba halmashauri ya kijiji imekubali kushindwa katika mvutano wa kimasirahi kati yake na uongozi wa kata na wilaya baada ya kulidhika kwamba hakuna nia thabiti ya kuiwezesha kujiendesha baada ya kunyimwa fursa kama zinazotolewa kwa vijiji vingine

Bw ntendeli amesema kuwa ikiwa  sababu hizo zilizotajwa hazitakuwa zimepatiwa ufumbuzi utakaokuwa umeulidhisha mkutano huo kabla ya  septemba 28 mwaka huu halmashauri ya kijiji cha kibondo mjini itatoa taarifa lasmi ya kujiuzuru nafasi yake kwa mkutano mkuu wa kijiiji hicho
Blog yako ya nguvu KIBONDO MOTO bado inafanya juhudi za kumtafuta mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya kibondo bw Leopord Chundu Ulaya ili kuzungumzia mwafaka wa  mgogoro huo kati ya serikali ya kijiji na halmashauri ya wilaya.

No comments:

Post a Comment