Pages

Tuesday, November 5, 2013

wazazi watakiwa kutambua faida ya elimu




Diwani wa kata ya kumsenga wilayani kibondo mkoani kigoma bw Saimon Kanguye ametoa wito kwa wazazi kutambua faida ya elimu ikiwa ni pamoja na  kujenga utamaduni wa kuwahimiza watoto wao kwenda shule kwa kuwa elimu ndio mkombozi wa masikini

Bw Kanguye ametoa wito huo katika mkutano wa hadhara aliouitisha katika kijiji cha Kibuye kata ya Kumsenga baada ya zahanati ya kijiji hicho kuwa na upungufu wa watumishi huku shule ya msingi ya kijiji hicho ikiwa haijawahi kuwa na mwalimu mzawa  

Bw Kanguye amesema kuwa kwa hivi sasa vijana wengi wamejiingiza katika swala zima la matumizi ya madawa ya kulevya hali inayosababisha kupoteza ndoto na malengo ya baadae hivyo wazazi wanapaswa kuwa makini ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha watoto wao juu ya athali za matumizi ya madawa ya kulevya

Kwa upande wake katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi wilayani kibondo bw Hamis Salumu Tahilo amesema kuwa wazazi wanapaswa kujitowa wakati wa kusomesha watoto kwa kuwa elimu ni biashara inayolipa baada ya miaka mingi

No comments:

Post a Comment