Pages

Monday, November 24, 2014

mbunge wa jimbo la muhambwe azuia wananchi kujiandikisha ili haki ipatikane





Mbunge wa jimbo la muhambwe bw Felix Mkosamali amezuia wananchi kujiandikisha kwa ajiri ya uchaguzi wa serikali za mitaa katika kituo cha sekondari murungu kijiji cha Kumuhasha akishinikiza halimashauri kuruhusu wananchi wa kijiji cha Nduta kambini kuruhusiwa kujiandikisha katika kituo hicho baada ya kutokuwa na kituo cha kujiandikisha kijijini kwao


Bw Mkosamali ametoa agizo hilo akiwa katika kituo hicho mapema hii leo novemba 24 , ambapo alikuta karani mwandikishaji akikataa kuwaandika wananchi ambao ni wakazi wa kijiji cha nduta kambini kwa madai kuwa ni maagizo aliyopewa na afisa mtendaji wa kijiji hicho


Aidha bw Mkosamali amesema kuwa wananchi wa kijiji cha Nduta kambini kama walivyo wananchi wengine wanahaki ya msingi kikatiba ya kuchagulia na kuchagua kiongozi wanayemtaka na kwamba hizo ni hujuma za chama cha mapinduzi wakitaka wananchi wa kijiji hicho wasipate fursa ya kuchagua na kuchaguliwa


Baadhi ya wananchi waliokumbwa na mkasa huo wamesema kuwa wameshindwa kujiandikisha baada ya kukataliwa kwa madai kuwa wao hawapaswi kujiandikisha katika eneo hilo kwa kuwa sio kijiji chao  


Kwa upande wake karani mwandikishaji wa kituo hicho bw Kadiri Hamidu amesema kuwa yeye anafuata maelekezo aliyopewa na afisa mtendaji wa kijiji hicho kwamba hapaswi kuwaandika wananchi wanaokaa nduta kambini


Nae afisa mtendaji wa kijiji cha kumuhasha bw meshaki mavukilo alipoulizwa swala hilo amesema kuwa maelekezo aliyopewa ni kuwa kila mwana kijiji anapaswa kujiandikisha katika kijiji anachokaa kwa maana hiyo wakazi wa nduta hawapaswi kujiandikisha katika kijiji hicho  



 msimamizi wa uchaguzi bw Fedi Eliasafi amesema kuwa wananchi wa kijiji cha Nduta kambini wanapaswa kujiandikisha katika vijiji walivyotokea kwa kuwa hakuna kijiji cha Nduta kambini na kwamba hakuna kituo cha kuandikisha wananchi katika kijiji hicho ENDS

No comments:

Post a Comment