Pages

Thursday, December 19, 2013

mgambo wahitimu mafunzo ya awli ya kijeshi





Wito umetolewa kwa wananchi wilayani kibondo mkoani kigoma kuendelea kusalimisha siraha ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za watu wanaomiliki siraha  kinyume cha sheria ili kuimarisha ulinzi na usalama miongoni mwa jamii

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya mgambo katika kata ya Kitahana na kuongeza kuwa raia wema wanaosalimisha siraha na  wanaotoa taarifa za watu wanaomiliki siraha hupewa motisha ya pesa isiyopungua shilingi elfu hamsini

Aidha bw Mwamoto amesema kuwa kwa yeyote anayetoa taarifa za watu wanomiliki siraha kinyume cha sheria au kusalimisha siraha hawawezi kuchukuliwa hatua yoyote ya kisheria badala yake atapewa motisha ili kusaidia upatikanaji wa siraha nyingine Zaidi

Vijana wapatao 94 wote wa kiume wamemaliza mafunzo ya awali ya mgambo  kati ya 165 walionza mafunzo hayo katika vijiji vya kibingo na Rusohoko kata ya Kitahana, mafunzo  yaliyoanza lasmi tangu July 1 mwaka huu Ends

No comments:

Post a Comment