Pages

Thursday, August 28, 2014

wakazi wa kibondo watahadhalishwa juu ya ugonjwa wa Ebola




Serikali wilaayani kibondo mkoani kigoma imewataka viongozi wa ngazi zote katika vijiji na kata kuhakikisha wanakuwa makini na kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutoa taarifa mapema pale watakapogundua  mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola

Maagizo hayo kwa viongozi wa vijiji na kata yametolewa na katibu tawala wa wilaya ya kibondo bw Ayubu Sebabili wakati wa maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika katika kata ya misezero hapo juzi August 26 ambapo alialikwa kama mgeni lasmi katika maadhimisho hayo

BW Sebabili amesema kuwa ni vema wananchi wakawa makini hasa ukizingatia kuwa wilaya ya kibondo ipo mpakani na tayari nchi jirani ya congo DRC imetangaza uwepo wa wagonjwa wa ebola katika nchi hiyo hivyo kuna uwezekano mkubwa wa watu kusafiri na ugonjwa huo hasa mipakani

Amesema viongozi wa vijiji na kata wanapaswa kuwa makini na kuelimisha wananchi juu ya ugonjwa wa ebola ikiwa ni pamoja na kuwapeleka wagonjwa wote wenye dalili za ugonjwa wa ebola katika zahanati iliyo karibu au kituo cha afya ili waweze kuchunguzwa na kupewa rufaa ya kwenda katika hospitali kubwa iwapo watakutwa na dalili au maambukizi ya ugonjwa huo

Bw Sebabili amesema kuwa kwa mjibu wa wizara ya afya dalili za ugonjwa wa Ebola ni pamoja na homa kali ya ghafla, kulegea mwili, maumivu ya misuli, kuuma kichwa, na vidonda kooni. Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha, vipele vya ngozi, figo na ini kushindwa kufanya kazi na kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa damu ndani na nje mwilini.ENDS

No comments:

Post a Comment