Pages

Monday, September 22, 2014

WAZAI WALEWA CHAKALI , WAMLALIA MTOTO WAKUTA AMEFARIKI DUNIA ASUBUHI

Mtoto anayekadiliwa kuwa na umri wa miezi sita amefariki dunia baada ya kulaliwa na wazazi wake wanaoishi katika kitongoji cha boma wilayani kibondo mkoani kigoma  ambapo inasemekana wazazi hao walikuwa wamelewa

Mwenyekiti wa kitongoji cha Boma bw Nuhu Kasiga amesema kuwa  baba wa mtoto huyo bw nshima buguru ambaye nae alikuwa amelewa  baada ya kugundua kuwa mtoto amefariki majira ya saa 10 za usiku aliamka na kwenda  kutoa taarifa  kwa mwenyekiti huyo kwamba mkewe aitwaye mary Antony amelalia mtoto akiwa amelewa na kusababisha kifo chake  


Amesema kuwa hatua za kipolisi zimefanyika ambapo mwili wa mtoto huyo ulichukuliwa na kupelekwa hospitali ya wilaya ya kibondo na mama wa mtoto huyo bi Mary Antony anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano Zaidi kuhusu tukio hilo la kusikitisha  


Katika tukio linguine ni kwamba Mwanamke mkazi wa kata ya Busunzu wilayani kibondo amefariki dunia baada ya kupigwa na radi katika nyumba ya mkazi wa kitongoji cha kolimba alipokuwa amejikinga mvua wakati akitokea  sokoni kijiji cha Nyakwi  mwishoni mwa wiki iliyopita

Kaimu afisa mtendaji wa kata ya Busunzu bw Shabani Mahamud Ruhinda amemtaja mwanamke huyo kuwa ni bi Salome Malora Mahangabili mwenye umri wa miaka 50  mkaziwa kitongoji cha mandela kata ya Busunzu wilayani kibondo 

Bw Ruhinda amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi September 19 majira ya saa saba mchana ambapo maama huyo baada ya mvua kunyesha aliamua kujikinga mvua kwa bw Godwin Ntambala wa kitongoji cha kolimba ndipo mauti yakamkuta baada ya kupigwa na radi


Amesema kuwa baada ya mvua kupungua watu wengine waliokuwa wamejikinga mvua pamoja katika nyumba hiyo walimuita ili waweze kuondoka na alipofika mlangoni alipigwa na radi na kufariki dunia papo hapo na kwamba kifo hicho hakijahusishwa na Imani zozote za kishirikina ENDS 

No comments:

Post a Comment