Pages

Saturday, November 30, 2013

mkuu wa wilaya ya kibondo agawa mbolea kwa wazee

bw Venance Mwamoto akisoma majina ya wazee wenye sifa za kupata mbolea hiyo



KIBONDO

Mkuu wa wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto amegawa mifuko 78 ya mbolea aina ya Minjingu kwa wazee wapatao 164 wa kijiji cha Kibuye Kata ya Kumsenga  aliyoikamata mwaka jana ikiwa kwenye harakati za kuvushwa nje ya nchi kwa njia za magendo

Bw Mwamoto amesema kuwa ameamua kutoa mbolea hiyo kwa wazee wa kijiji cha Kibuye kwa kuwa ilikamatiwa kijijini hapo mwaka jana kabla ya kuvushwa kwenda nchi jirani ya Burundi ikiwa ni kwa njia za magendo ‘’ nimeamua kugawa mbolea hii kwa wazee kuwa kuwa wao kwanza hawana nguvu na itawasaidia kuboresha mashamba yao na kuongeza kipatocha familia’’ alisema mwamoto 

Bw Mwamoto amesema kuwa ameamua kugawa mifuko 74 kwa wazee kisha kubakiza mifuko mingine minne ya mbolea hiyo kwa ajili ya ushahidi kwa watu wa TAKUKURU pamoja na polisi kama itahitajika kufanya hivyo kwa upelelezi Zaidi wa wahusika wa wizi wa mbolea hiyo

Bw Mwamoto amesema  kuwa alikamata mbolea hiyo mwaka jana mwezi wa katika kijiji cha Kibuye kata kumsenga ikiwa kwenye harakati ya kuvushwa kwenda nchi jirani ya Burundi kwa ajiri ya kuuzwa huko pamoja na kwamba mbolea hiyo ilitolewa kama ruzuku kwa wananchi wa wilaya ya kibondo  

Mmoja wa wazee hao bw Charles Ntambala amesema kuwa amefurahishwa na zoezi hilo na kwamba litakomesha wizi wa mbolea ambao umekuwepo kwa muda mrefu na kusababisha wanyonge kutopata haki yao ya msingi kutokana na kuuzwa kwa matajiri wa nchi jirani ‘’ kama unavyojua ndugu mwandishi hapa ni mpakani mbolea imekuwa ikifanyiwa magendo kwa muda mlefu sana na kusababisha sisi tukose haki yetu ya msingi kutokana na mbolea kuongezeka bei maradufu kutona na kuuzwa nje ya nchi namshukuru sana mkuu wa wilaya haijawahi kutokea tangu niishi kijii hiki’’ alisema mzee huyo  

Bw mwamoto amesema kuwa zoezi la ukamataji mbolea inayofanyiwa magendo litakuw aendelevu ili kukomesha wizi huo unaosababisha wananchi wakose haki yao ya msingi na kudumaza maendeleo kwa watanzania ENDS 






No comments:

Post a Comment