Pages

Friday, October 19, 2012

kamati ya amani yaundwa wilayani kibondo kusaidia kuzuia machafuko ya kidini



KIBONDO
Mkuu wa wilaya ya kibondo mkoani kigoma bw Venance Mwamoto ameunda kamati ya amani inayohusisha viongozi wa dini za kiisilamu na kikiristo ,vyama vya siasa pamoja na viongozi wa serikali ili kutokomeza uvunjifu wa amani unaofanywa na wahalifu wanaotumia mgongo wa madhehebu mbali mbali

Katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa vijana wilayani kibondo wajumbe 17 wamechaguliwa kuongoza kamati hiyo ambapo wajumbe hao wametoka katika mathehebu mbali mbali ya kikiristo na kiislamu pamoja na vyama vya siasa

Mkuu wa wilaya ya kibondo bw Mwamoto amesema kuwa kamati hiyo ya amani itasaidia kutatua kero mbali mbali zinazoanzishwa na watu binafsi huku wakitumia mgongo wa dini au dhehebu Fulani na kusababisha vurugu zisizokuwa na msingi miongoni mwa jamii

Akiongea katika mkutano huo wa kuchagua kamati ya amani bw Mauld Juma ambaye ni mkazi wa kibondo mjini ameshauri kamati hiyo ihakikishe makosa yanayofanywa na waumini wa kikirosto au kiisilamu wanayabeba wao wenyewe na si kuyageuza ya kikundi au dini Fulani

Kamati hiyo ya amani imeungwa mkono na viongozi wa madhehebu hayo ya kikiristo na kiislamu na kwamba imeundwa ili kulinda amani iliyopo wilayani hapa na  kuzuia fujo zinazoweza kutokea ambapo siku za hivi karibuni kumekuwa kukitokea fujo zinazotokana na visa vya kidini  MWISHO

No comments:

Post a Comment